Saturday, June 27, 2015

Mashindano ya serikali za mitaa manispaa ya mtwara yapamba moto

Mashindano ya serikali za mitaa manispaa ya mtwara yapamba moto kwa kupatkana kwa timu 4 za kucheza nusu fainal za patkana hapo Jana!!!! Ungana nami hapo baadae kwa taarfa zaid

Monday, March 23, 2015

SIMBA YA STEMMUCO YAIRARUA YANGA

 Klabu ya soka ya Simba ya STEMMUCO, imedhihirisha kuwa siku zote Yanga hafurukuti pindi akutanapo na Simba, baada ya kuinyuka kipigo cha mbwa mwizi, magoli 6-1. Katika mchezo wa kirafiki uliojaa ufundi na burudani ya aina yake, uliyoishuhudia timu ya Yanga ikizabwa magoli hayo mapema kunako sekunde ya 18 kupitia kwa Benjamin a.k.a OKWI, aliyeonekana kuwa mwiba wa timu pinzani, kwani aliweza pia kuipatia Simba magoli katika dakika ya 38 na 64 na kung'ara kama mchezaji bora wa mcezo. Magoli mengine ya Simba yalifungwa na Masoud dakika ya 47, Khamis dakika ya 71 na White dakika ya 85, wakati bao pekee la Yanga likifungwa na Ligwa dakika ya 5. Hadi mwisho wa mchezo huo, Simba ilitoka uwanjani huku ikiwa na utajiri huo wa magoli.



 
MASHABIKI WAZALENDO WA STEMMUCO, WALIJITOKEZA PIA KUKITIZAMA KIPUTE HICHO KWANI HAWAKUTAKA KABISA KUSIMULIWA

WACCHEZAJI WA SIMBA, WAKIPONGEZANA BAADA YA KUFUNGA MOJA YA MAGOLI

MCHEZAJI WA SIMBA BENJAMINI, AKISHANGILIA KWA 'KUSLAIDI' KWENYE NYASI ZA UWANJA HUO, HUKU AKIPONGEZWA NA WACHEZAJI WENZAKE BAADA YA KUFUNGA GOLI

WACHEZAJI WA TIMU YA SIMBA WAKIMSIKILIZA KOCHA WAO, LUAMBANO. KABLA YA KUREJEA DIMBANI KWA AJILI YA KIPINDI CHA PILI


KIKOSI CHA TIMU YA SOKA YA YANGA ( STEMMUCO)
BAADHI YA MASHABIKI WA YANGA, WAKIWA NA NYUSO ZA HUZUNI
TIMU YA YANGA IKIWA KATIKA MAPUMZIKO YA KIPINDI CHA KWANZA
MCHEZAJI WA YANGA, KAPAMA WA PILI KULIA, AKIMSHURUTI MWAMUZI, KUMUONESHA KADI YA NJANO BENJAMIN WA KWANZA KULIA, BAADA YA KUVUA FULANA WAKATI AKISHANGILIA GOLI LAKE LA TATU.
HAUKUWA MPAMBANO WA OSEA NA KIDARA PEKEE, HATA NYASI ZA UWANJA WA SHULE YA MSINGI SHANGANI ZILIKUWA KATIKA WAKATI MGUMU.
MASHABIKI WALIOPENDEZA NYUSO, BILA SHAKA HATA MIFEREJI YA NYOYO ZAO, WALIFIKA PIA KUSHUHUDIA PAMBANO HILO LA KUKATA NA SHOKA





                               

                                         " AUNGURUMAPO SIMBA, HUCHEZA NANI?"

                                             IMEANDALIWA NA; ALBINUS GREGORY






Friday, January 23, 2015



TANGAZO   TANGAZO  TANGAZO
Ni kwa mara nyingine mashindano ya BIG SCORE yanafikia kilelee siku ya jumamosi baada ya hatua ya makundi kumalizika. Kwenye football leo tar 23/01/2015 siku ya ijumaa kutakuwa na mechi ya nusu fainali kati ya mwaka wa pili B a.k.a Fighter’s FC dhidi ya mwaka wa pili A a.k.a Alliance FC, mechi itachezwa majira ya saa 8:00 mchana kwenye kiwanja cha jeshini. Mida ya saa 10:00 jioni vijogoo wa mwaka wa tatu watapambana wa mwaka wa kwanza kwenye kiwanja cha jeshini. Fainali itachezwa tar 25/01/2015 kwenye viwanja vya TTC
Netball:
Baada ya mzunguko kumalizika sasa wadada wa mwaka wa pili wanakutana uso kwa uso na wadada wa dip&cet katika mechi ya fainali tar 25/01/2015
Katika viwanja vya TTC . Je wadada wa dip&cet watalipa kisasi kwa kichapo cha mara ya kwanza walichopata kutoka kwa dada zao wa mwaka wa pili? Karibu ujioneee
       Basketball
Baada ya mzunguko sasa mwaka wa pili ambao ndo mabingwa watetezi wataminyana na mwaka wa tatu katika mechi ya fainali itakayofanyika siku ya Jumamosi katika kiwanja cha Bandari Club majira ya saa 10:00 jioni. Je mwaka wa pili wataendeleza ubabe wao wa kutofungwa na madarasa mengine? Karibu ujionee
WOTE MNAKARIBISHWA SANAAAAAA .