Saturday, September 21, 2013

IMPORTANT DATES FOR REPORTING AND REGISTRATION

All students both new and continuing in various programmes are required to read, understand and abide by the instructions below.

IMPORTANT DATES FOR REPORTING AND REGISTRATION

Programme Date of Arrival Undergraduate (First Year) 16th September 2013, Undergraduate (Continuing) 23rd September 2013 Masters (MBA-Evening) 16th September 2013 Masters (MEMP-Weekend) 20th September 2013 Diplomas and Certificates 15th October 2013
The registration for all new students shall start from 9.00 a.m. EXCEPT those for MEMP-Weekend) programmes are who shall report from 2.00 p.m.
                                 

REQUIREMENTS FOR REGISTRATION

 All selected students shall be registered after fulfillment of the following:
    A. FEES PAYMENT
           (i) No student shall be allowed to register or attend classes unless the required fees have been paid as shown in the fee structure (Visit  www.stemmuco.ac.tz).

          (ii) Bring with you the Original pay-in slip. Cheques, cash, faxes, scanned pay-in slips, emails of                         confirmation of payments and any other form of payments are not acceptable.

          (iii) Fees paid will not be refunded if a student withdraws or leaves the University without permission.

          (iv) However, if a student receives prior permission from the Deputy Principal for Academic Affairs                    (DPAA) to withdraw or to be away from the University and provided that the application in writing                 to withdraw or to be away from the University is submitted within two weeks of the academic                       year or semester, fifty percent (50%) of the fees may be refunded.

 B. DOCUMENTS FOR REGISTRATION
          (i) Note your Course Programme.

          (ii) All students must bring Original Degree Certificates and/or Original Transcripts (For masters                         students), Original Certificates of Form Six, Form Four and Diploma/Certificate and Original Birth                Certificate. Note: Photocopies, downloaded internet results, faxes, affidavits and certified results are               not acceptable.
          (iii) Students shall be registered under the names appearing in the Certificates they submitted for the                     application. No change of names shall be accepted unless all requirements provided under                             STEMMUCO Students’ By-Laws have been observed.

           (iv) Students are advised to register for the course programme, which they have been admitted.

  C.  DURING AND AFTER REGISTRATION
        i) No student shall be allowed to postpone studies after the academic year has begun except under                  special circumstances. Permission to postpone studies shall be considered after the student has                      produced satisfactory evidence of the reasons for postponement to the DPAA. Special                                  circumstances shall include ill health or serious social problems.

       (ii) No students shall be allowed to postpone studies during the two weeks preceding final                                 examinations, but may for valid reasons be considered for postponement of examinations.

       (iii) Students shall commit themselves in writing to abide by the University’s Rules and Regulations as                 required in the registration form. A copy of the students Rules and Regulations shall be made                         available to the student through the office of the Dean of Students. Students are encouraged to                       read and abide by them.

       (iv) Students shall be issued identification cards, which they must carry all times and which shall be                      produced when demanded by appropriate University Officers. The identity card is not                                  transferable and any fraudulent use may result in loss of student privileges or suspension.

       (v) Loss of the identity card should be reported to the Office of the Director of Postgraduate                              Studies, where a new one can be obtained after paying an
                 appropriate fee (currently Tshs 10,000/=) as stipulated under STEMMUCO Rules and                                Regulations.

        (vii) Any late registration (two weeks after reporting date) is liable to a penalty of Tshs 100,000/= 

D PAYMENT OF FEES
      All prescribed fees shall be paid directly to Stella Maris Mtwara University College. Account                           Name: SAUT-TUITION FEE, Account No: 0151054341502 CRDB BANK (LTD) MTWARA                         BRANCH.

                                                               Mahiza Danstan
                                                      Deputy Minister of Information
                                                                 STEMMUSO
    

Monday, September 9, 2013

Supplementary & Special University Examinations;

Dear Students of Stella Maris Mtwara University College you are hereby informed that for those students who had supplemented in their second semesters University Examinations or for those having the related problems you should have to follow the following instructions;-

1. Supplementary and Special University Examinations shall be done during the next week of 16th - 21st September 2013. Failure to attempt the exams without prior information with undue reasons, the offense shall attract to discontinuation of the Studies subject to the Saint Augustine University of Tanzania's Examination's regulations.

2. There wont be an ample time for sitting for exams to those who shall have missed the exams in accordance to the timetable therefore walk on time to avoid unnecessary difficulties in your academic matters.

3. For having the special cases in matters related to exams should appear in person to the examination's officer for further assistance.

4. Lastly you are instructed to solve your academic matters (If any) by using the proper channels and not otherwise!

                                                           Danstan Mahiza

                              Deputy minister of Information
                                             STEMMUSO

Wednesday, July 10, 2013

Dr.Kitima Astaafu uongozi SAUT

                      
                          



PADRI Daktari Charles Kitima alipoteuliwa kuwa makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Mt Agustino (SAUT), Mwanza mwaka 2004, hakuna aliyekuwa na wazo kwamba miaka kumi ya uongozi wake angeweza kufanya maajabu ya kukifanya chuo hicho kuwa hivi kilivyo.

Akishika nafasi ya mtangulizi wake, Monsinyori Dakta Deogratias Rweyongeza, aliamini kuwa amepewa kazi kubwa na nzito katika taifa. Nayo ni kupigana na moja ya maadui wakubwa ‘ujinga’. Hivyo, aliazimia kutumia nguvu, akili, maarifa na wakati mwingine kuteseka kwa ajili ya maendeleo ya chuo hicho.


Kasi yake ndiyo inayowashangaza wengi ndani ya kanisa na nchi kwa ujumla, ambapo atakapokabidhi madaraka kwa mwenzake Julai mwaka huu, Padri Kitima anaicha SAUT ikiwa ndicho chuo kikuu pekee nchini chenye idadi kubwa ya wanafunzi, matawi mengi na maendeleo ya kuridhisha.


Chuo Kikuu cha SAUT kilianzishwa rasmi mwaka 1998 ikiwa ni mafanikio ya kilichokuwa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Nyegezi (Nyegezi Social Training Institute) kilichoanzishwa tangu mwaka 1960 na Wamisionari wa Kanisa Katoliki ambao kwa sasa wanajulikana kama Wamisionari wa Afrika chini ya Askofu Mkuu Joseph Blomjous wa Jimbo Kuu la Mwanza.


Mwanzoni mwa miaka ya 1960 kilikuwa ni kipindi ambacho nchi nyingi za Afrika zilipata uhuru ikiwemo Tanzania. Kutokana na wimbi la mabadiliko katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara, Wamisionari wa Afrika walitambua kuwa ujuzi katika suala la habari na mawasiliano, maendeleo ya jamii, uhasibu, usimamizi na utawala vilihitajika kuendelezwa ili kuelimisha wafanyakazi ambao wangechukua uongozi katika nchi za Afrika Mashariki na Kati ambazo zilikuwa zimepata uhuru.


Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Nyegezi (NSTI) ililenga kutoa mafunzo ya kitaaluma na kitaalamu, lakini pia kutoa maadili ya elimu ya uraia na kijamii kwa wazawa bila kujali rangi au imani katika nyanja hizo kuu za elimu.


Askofu Joseph Blomjous alipostaafu mnamo mwaka 1964, alikabidhi taasisi kwa mrithi wake, Askofu Renatus Butibubage ambaye aliongoza taasisi hii hadi mwaka 1975 alipoikakabidhi rasmi kwa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).


Hadi kufikia mwaka 1998 zaidi ya watu 2,400 walikuwa wamepata mafunzo katika taasisi hii kwa ajili ya kutoa huduma katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.


Tangu mwaka 1992 kulikuwa na hoja mbalimbali ndani ya Serikali ya Tanzania, ikiwamo suala la utoaji wa huduma za kijamii kuwa huria. Hivyo mwaka 1996 ukawa mwaka kikanisa ulioazimia kupanua huduma ya elimu ya chuo kikuu.


Hivyo, Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Nyegezi, ikapandishwa hadhi na kuwa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (St. Augustine University of Tanzania-SAUT), chini ya TEC kikikubali mamlaka ya sheria ya Canon (Canon Law) na katiba ya Apostoliki (Apostolic-Constitution) “Ex-Corde Ecclesiac” kwa ajili ya vyuo vikuu Katoliki.


Chuo cha Mtakatifu Augustino kimeanzishwa kwa mujibu wa sheria za nchi na kinafanya kazi chini ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa mujibu wa masharti ya vyuo vikuu sheria namba 7 ya mwaka 2005.


Haikushangaza kuona kwamba ndani ya muda mfupi wa uongozi wa Kitima, mamia ya wanafunzi kutoka nchi nyingi za Afrika Mashariki kama vile Kenya na Uganda pamoja na za bara la Ulaya, Amerika, na Australia walivutiwa sana kuja kusoma katika chuo hiki.


Dira na maono


Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania waliamua kupanua huduma ya utoaji wa elimu ya juu katika maendeleo ya mtu na heshima kwa utu wa binadamu.

Lengo la kuanzishwa kwake


Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kililenga kuwa kituo cha ubora wa elimu, utafiti na utumishi wa umma; kukuza harakati na ulinzi wa kweli, uwazi na uaminifu, pamoja na umahiri na kujituma katika utoaji huduma; kujenga na kuendeleza dhamira ya kutunza mali binafsi na mali ya umma; kuhamasisha maendeleo ya jumla kwa kutoa elimu bora juu ya uwezo wa uchambuzi na dhamira ya kutoa huduma kwa ukarimu na heshima kwa binadamu.

Mafanikio yake tangu 1998


SAUT kilipoanza mwaka 1998 kimefanikiwa chini ya uongozi wa Padri Kitima, kimeongeza matawi mengine mapya 13 katika kanda mbalimbali hapa nchini, na kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 204 hadi 13,121 kwa mwaka wa masomo 2012/2013.
Chuo kimeongeza vitivo vingine vinne (4) kutoka kitivo kimoja cha Sayansi ya Jamii na Mawasiliano ambacho kilikuwa na shahada moja ya Mawasiliano ya Umma. Kimefanikiwa kujenga madarasa mapya, na majengo ya utawala ambayo yamesaidia sana kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu bora.

Chuo kimefanikiwa kutoa elimu kwa wazawa juu ya kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za kuishi wanafunzi (hostel) ambazo zimewawezesha kujipatia kipato na pia kuwapa elimu ya biashara ndogondogo.


Kinachofundishwa SAUT


Tangu chuo kuanzishwa mnamo mwaka 1998 kumekuwa na ongezeko la programu mbalimbali ambazo zimekuwa zikiongezwa kwa awamu tofauti. Hii ni kutokana na tafiti makini na za kina zinazofanywa na wahadhiri wa chuo ndani na nje ya nchi, ambazo zimekisaidia kutambua umuhimu na uhitaji wa programu mbalimbali katika maendeleo ya jamii, Afrika na duniani kwa ujumla. Programu hizi zimegawanyika katika vitivo vifuatavyo:

Kitivo cha biashara na utawala:


Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Biashara, Sayansi katika Ugavi, Utalii na Usimamizi. Nyingine ni Stashahada ya Juu katika Ununuzi na Usimamizi katika Ugavi na Uhasibu. Pia kinatoa elimu ya cheti katika Utawala wa Afya na Ugavi.

Kitivo cha Sayansi ya Jamii na Mawasiliano:

Hiki kinatoa elimu ya Shahada ya Uzamivu katika Mawasiliano, Uchumi, Mawasiliano ya Umma na Maendeleo ya Jamii. Kinatoa pia Shahada ya Mawasiliano ya Umma na Masoko, Uchumi, na Maendeleo ya Jamii. Kadhalika kinatoa elimu ya cheti katika Uandishi wa Habari.

Kitivo cha elimu:

Kitivo hiki kinatoa elimu kiwango cha Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Mipango ya Elimu, Usimamizi wa Maendeleo ya Elimu ya juu na katika Isimu.
Pia kinatoa Shahada ya Sanaa na Elimu, Shahada ya Falsafa na Elimu na Shahada ya Mafunzo ya Dini na Elimu.

Kitivo cha Sheria:


Kwa sasa kitivo hiki kinatoa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Sheria, na Shahada ya Uzamili katika Sheria. Kadhalika kinatoa Shahada ya Sheria.

Kitivo cha Uhandisi:


Hiki kinatoa elimu ngazi ya Shahada ya Sayansi katika Uhandisi Ujenzi, Shahada ya Sayansi katika Uhandisi Umeme pamoja na cheti katika Teknolojia ya Habari.

Changamoto


Wahenga wanasema “kwenye msafara wa mamba na kenge hawakosekani”, ndivyo ilivyo katika Chuo cha Mtakatifu Augustino, kwani pamoja na mafanikio yaliyopatikana tangu kilipoanzishwa yapata miaka 14 sasa, kumekuwa na changamoto mbalimbali. Hizi ni pamoja na ucheleweshwaji wa malipo ya ada kwa wanafunzi wanaolipiwa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.

Changamoto hii imekuwa ikijitokeza kila mara na kwa muda mrefu hali ambayo imesababisha chuo kuchelewa kutekeleza baadhi ya shughuli za maendeleo ya elimu.


Nyingine ni kuyumba kwa uchumi wa taifa usio imara, na ushawishi wa kisiasa ambao unaweza kuharibu uhuru katika utoaji wa elimu.

Kadhalika kipato cha chini kwa Watanzania walio wengi kunachangia baadhi ya wanafunzi kushindwa kumudu gharama za masomo ya elimu ya juu hivyo kushindwa kuendelea na masomo.

Mafanikio


Dk. Kitima alipoulizwa amewezaje kufanikisha haya ndani ya muda mfupi hadi chuo kikawa na umaarufu kiasi hicho anasema: “Siri ya hatua hii nzuri iliyofikiwa na SAUT inatokana na ubora wa elimu inayotolewa na chuo kwa kuangalia mahitaji muhimu yanayomwezesha mwanafunzi kuwa na uwezo na ufanisi mkubwa wa kujiajiri na kuajiriwa baada ya kuhitimu.

“Katika mtaala wa chuo, wanafunzi wanapata fursa ya kusoma masomo ya ujasiriamali na kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao na hivyo kuondokana na dhana ya kungoja kuajiriwa.”


Anadai kuwa chuo kimeboresha kiwango cha elimu inayotolewa ili kuhakikisha wahitimu wanahimili soko la ushindani Afrika Mashariki na duniani kote, pia kutokana na elimu ya dini na maadili kwa wanafunzi wote.


“Lengo ni kusaidia kujenga maadili mazuri katika jamii kwani sasa upo mmomonyoko mkubwa wa maadili katika ofisi mbalimbali na kukithiri kwa rushwa, ufisadi na mengine mengi sambamba na hayo,” anasema.


Pia wanafunzi wote wanapata fursa ya kusoma masomo mbalimbali yanayomwezesha mwanafunzi kuwa na uwezo na ufanisi mkubwa wa kupambana na kukabiliana na mambo mbalimbali katika utendaji wa kazi, kama vile Kifaransa, Falsafa, Kiingereza, Ujuzi katika mawasiliano, Upembuzi yakinifu (Kufikiri kwa kina), Takwimu na Uchumi.


Ushirikiano na jamii


Chuo kimefanikiwa kuwawezesha wanajamii wa Kata ya Mkolani, hususan Kijiji cha Sweya ambapo kimewafadhili kupitia kikundi chao cha Muungano katika shughuli zao za ujasiriamali. Kila mwaka chuo hutoa kiasi cha shilingi milioni 20 kwa kikundi hicho.

Kimefanikiwa kutoa misaada ya vitabu mbalimbali kwa baadhi ya shule za msingi zilizo karibu na mazingira ya chuo kupitia shughuli mbalimbali za kitaaluma zinazofanywa na wanafuzi kwa jamii.


Chuo kimefanikiwa kutoa mafunzo ya maadili kwa wanafunzi wote, ambayo ni msaada mkubwa kwao katika utendaji wa kazi hasa katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia.


Kimefanikiwa na kinajivunia kuanzisha mashindano ya mpira wa miguu, mpira wa pete, kikapu, meza na riadha yajulikanayo kama “PRO-LIFE” (Promote Life) kuanzia mwezi Agosti hadi Februari kila mwaka.


Pia mashindano ya FAWASCO kuanzia mwezi Machi hadi Juni. Mashindano haya yanajumuisha jumla ya shilingi milioni 40 pamoja na fursa ya kutembelea nchi mbalimbali za Afrika Mashariki kwa mshindi wa kwanza na wa pili.


Chuo pia kimefanikiwa kuanzisha kituo cha kuzalisha na kuwawezesha wajasiriamali (Business Incubation Centre) ambapo wanafunzi wanaohitimu wanapata fursa ya kuandika mawazo yao ya biashara na baada ya mawazo yao kukubalika wanapatiwa mafunzo maalumu juu ya mawazo yao ya biashara na kisha wanapatiwa mtaji kati ya shilingi milioni 25 hadi 30 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali.


Wito kwa wadau


“Tunaiomba serikali kuandaa mazingira bora hasa kwa wahitimu kwa kuwapa mikopo stahiki kupitia asasi za serikali kama benki ili waweze kutumia ujuzi walionao hasa kiujasiriamali na kuleta maendeleo kwa mtu binafsi na taifa kwa ujumla.
“Tunaishauri serikali na sekta binafsi kuwatumia wasomi mbalimbali katika mipango ya maendeleo ya nchi ili wananchi waweze kufaidi matunda ya wasomi kwa maendeleo ya taifa,” anasema Dk. Kitima na kuongeza:
“Serikali pia inapaswa kuboresha elimu ya msingi na sekondari ambayo haswa ndio kitovu cha ubora wa elimu, ili kusaidia taasisi za elimu ya juu kupata wanafunzi wa kutosha na wenye sifa sitahiki.”
Anasema serikali inapaswa kuviangalia vyuo binafsi na kuviwezesha angalau kwa kuvipatia ruzuku kwa ajili ya miradi yake ya maendeleo, kwamba hii itasaidia kuongeza kasi ya maendeleo na kukuza ubora wa elimu ya juu hapa nchini.
“Serikali inapaswa kutimiza wajibu wake wa kutoa mikopo kwa wakati ili kuepuka migomo na maandamano yasiyo na tija kwa jamii,” anasema na kuwataka wananchi wawe mstari wa mbele kuwekeza katika elimu ya juu kwa kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo na si kuwaachia watu wa nje au nchi jirani kufanya hivyo.
Kwa upande wa wananchi, anashauri wakazi wa Kanda ya Ziwa hususani Mkoa wa Mwanza, Wilaya ya Nyamagana mahali ambapo chuo kipo, kushirikiana nacho katika kuwalea na kuwahudumia wanafunzi kwa malazi na ulinzi ili kudumisha amani na mshikamano.
“Tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuendeleza ushirikiano katika suala la ulinzi na usalama katika eneo la chuo na sehemu za makazi ya wanafunzi wetu ili waweze kusoma kwa amani na utulivu.
“Tunatoa wito kwa wafanyabiashara na wawekezaji mbalimbali kukiunga mkono chuo chetu katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile ujenzi wa madarasa, vifaa vya kufundishia kama vile kompyuta na vitabu mbalimbali.
“Tunatoa wito kwa wanafunzi wote wa SAUT wawe na moyo wa upendo na kujali mali za chuo, pia washiriki vyema katika shughuli za kitaaluma na michezo ili kutunza heshima ya chuo ndani na nje ya nchi,” anasema.
Anatoa wito kwa wahadhiri wote wa SAUT kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia dira ya chuo ambayo ni kuendelea kuwa kituo cha ubora na mafanikio katika elimu ya juu na huduma kwa jamii.

                                                               Mahiza  Danstan
                                                           Naibu Waziri wa Habari
                                       Stella Maris Mtwara University College

Thursday, June 13, 2013

Attention to STEMMUCO Graduands of the year 2011/2012.

Get visit to http://www.stemmuco.ac.tz and get the important information that concern you!

Mr. MAHIZA, Danstan
The Deputy Minister for Information and College Affairs

YAH: MKUTANO WA II WA BUNGE LA SERIKALI YA WANAFUNZI STEMMUCSO

Hii ni kuwataarifu waheshimiwa wabunge, mawaziri na manaibu mawaziri, kwamba kesho Ijumaa June 14, 2013 saa mbili asubuhi, katika ukumbi wa MTR 8 Kutakuwepo na Mkutano wa II wa Bunge la Serikali ya Wanafunzi STEMMUCSO. Hivyo basi unaombwa kufika mapema bila ya kukosa ili Mkutano uanze kwa muda rasmi.

Imetolewa na Ofisi ya Bunge - STEMMUCSO.

Saturday, February 23, 2013

YAH: KUTEULIWA KWA PADRE TITUS MDOE (DPAF -STEMMUCO)

Kwa furaha kubwa na isiyo na kifani ninapenda kuchukua nafasi hii kuutaarifu umma wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Stella Maris Mtwara kwamba, Mheshimiwa Baba Padre Titus Joseph Mdoe wa Jimbo Katoliki la Tanga -Tanzania, ambaye alikuwa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Stella Maris Mtwara akishughulikia masuala ya Fedha, Utawala, na Mipango, ameteuliwa na Baba Mtakatifu Benedict XVI kuwa Mhashamu Baba Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam!
Utaratibu wa Kumuaga Baba Askofu Mdoe unaendelea kupangwa na Utawala wa Chuo, na Umma utafahamishwa kuhusu taratibu zote zitakazoendelea hapo baade.

Wenu katika ujenzi wa STEMMUCO

Ndg. KAMILI, John C.
Rais - Serikali ya Wanafunzi STEMMUCO.

Saturday, October 27, 2012

RE: THE OFFICIAL BEGGINING OF THE 2012/2013 ACADEMIC YEAR.

This is to inform the public of Stella Maris Mtwara University that, the Academic year for the year 2012/2013 has already started from 24th October 2012. You are advised to get in touch with the timetable of the University College as the studies are on progress and other activities are continuing as usual.
Welcome to STEMMUCO and get in touch with your Government.

SALLA, Donati P.
The Vice President.
STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

Friday, October 12, 2012

FOR THIRD YEAR STUDENTS ONLY WHO HAVE FINISHED THEIR STUDIES IN 2011/2012 ACADEMIC YEAR.

This is to inform the third year students who have finished their studies in the 2011/2012 Academic year that your academic results from first up to sixth semester are out and they are available to the University College's link which is Https://www.stemmuco.ac.tz If you have not yet settled the matters about research project  you can also visit the highlighted site and see the timetable for defending your research work.
If you will be having any query which shall rise as the effects of viewing your results you may send your matter directly to the following E-Mail addresses;-
(a) mpmandalu@yahoo.com
(b) sr.flora71@yahoo.com
(c) education.stemmuso@gmail.com

Thank you for visiting our blogsite.

SALLA, Donati P.
THE VICE PRESIDENT
STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

Re:THE RELEASE OF SUPPLEMENTARY/SPECIAL EXAMINATIONS.

This is to inform the public of Stella Maris Mtwara University College that, the results of Special/Supplementary Examinations which were conducted from 03rd September 2012 - 08th September 2012 are out and they are available in the University College Website which is Https://www.stemmuco.ac.tz if you are concerned with this information you may visit the highlighted link and see you results in the portal written "Combined Supp". For any query  you may send your matter direct to the following emails;-
(a) mpmandalu@yahoo.com
(b) sr.flora71@yahoo.com
(c) education.stemmuso@gmail.com

Thanks for your visit in this blogsite.
SALLA, Donati P.
THE VICE PRESIDENT
STEMMUCO.

Wednesday, September 19, 2012

YAH: WANAFUNZI WALIOSHINDWA KUFANYA MITIHANI MAALUM NA YA KUJAZILIA (SPECIAL & SUPPLEMENTARY EXAMINATIONS)

Baada ya Kikao Cha Kamati ya taaluma ngazi ya Chuo kukaa na kuamua maamuzi yake Mnamo wiki iliyopita, kikao hicho kimeamua maamuzi yafuatayo kwamba, wale wote walioshindwa kufanya mitihani tajwa hapo juu kutokana na sababu mbalimbali watapewa nafasi ya kufanya mtihani husika mnamo mwezi septemba 2013 kwenye kipindi cha kufanya mitihani maalum na ya kujazilia. Pamoja na hayo wanafunzi wafuatao wawasiliane na Ndg. Clement Francis - Naibu Waziri wa Habari na Masuala ya Chuo ili waweze kupata barua zao zinazohusiana na tangazo hili. Unaweza kuwasiliana na Ndg. Clement Francis kwa namba zifuatazo 0717 521230.
Wanafunzi hao ni;-
1. MSANGI, Ridhwan E. BAED 15283.
2. NYARUBONA, Kassim BAED 15430
3. RUTEMBA, Issa H. BAED 15531
4. MWAKUBALI, Jophrey BAED 21666
5. MILANZI, David BAED 21589.
6. KAYEGEJI, Adam K. BAED 14929
7. JACKSON, Mussa BAED 14803.

ANGALIZO: Wahusika wa tangazo hili ni wale wenye tatizo tajwa kuanzia Mwaka wa Kwanza hadi Mwaka wa Tatu. Kwa Msaada zaidi wasiliana na Mwadili - Kitivo Cha Elimu kwa simu Namba 0715 86 43 79.

CLEMENT Francis 
NAIBU WAZIRI WA HABARI NA MASUALA YA CHUO.
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.

Saturday, September 8, 2012

YAH: KUTOLEWA KWA TAARIFA RASMI NA YA MWISHO KUHUSU MPANGILIO WA VITUO VYA KUFANYIA MAZOEZI YA UALIMU (TP ALLOCATIONS)


Hii ni kuwataarifu wanafunzi wote wa Mwaka wa Kwanza ambao wanatarajia kuingia Mwaka wa Pili, na wale wa Mwaka wa pili wanaotarajia kuingia Mwaka wa tatu katika Mwaka wa Masomo 2012/2013 katika  Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara kwamba, taarifa rasmi ya matokeo ya kupangwa kwenye vituo vya kufanyia mazoezi ya Ualimu (Teaching Practices) inapatikana katika wavuti ya Http://www.stemmuco.ac.tz hivyo basi unapaswa kufungua wavuti tajwa ili ufahamu ni wapi ulipopangwa kufanya Mazoezi ya Ualimu.
NB: (1)Hapatakuwepo na mabadiliko yoyote ya Kituo hivyo basi NENDA KWENYE KITUO ULICHOPANGIWA MOJA KWA MOJA. Pia hupaswi kuchelewa kwenye Kituo kwa sababu kama Mtathmini atapita katika kituo chako na akakukosa  utapaswa kurudia mwaka wa masomo kwani TP ni sehemu ya mtihani wa kitaaluma hapa Chuoni.
(2) Kwa tatizo lolote litakalo jitokeza wakati ukiwa kwenye mazoezi  unapaswa kuwasiliana na Mratibu wa eneo lako au kupiga namba za simu zifuatazo 0713 286 999, 0717 521230
, 0765 194 201. 
(3) Baada ya kumaliza Mazoezi unapaswa kuja Chuoni Moja kwa Moja kwa ajili ya Masomo kama ratiba inavyoelekeza. (Kwa Maelezo kuhusu tarehe za kufungua Chuo pekua katika Masjala ya wazi ya blogu hii).

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais.
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.

YAH: HOSTELI ZA CHUO.

Hii ni kuutaarifu Umma wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara kwamba Hosteli za Chuo katika mwaka wa masomo 2012/2013 ni kwa ajili ya Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza tuu na wale wanafunzi wenye Mahitaji maalumu. Hivyo basi wale walioshikilia vyumba kwa kuvifunga na kuondoka na funguo za vyumba husika wanapaswa kurudisha mara moja kwa Kiongozi Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Udahili, Ukaribisho, na Makazi kwa namna yeyote ile na kwa haraka itakavyowezekana. Wale wanafunzi wenye mahitaji maalum watume barua za maombi ya kuishi hosteli kwenda kwa Mwadili wa Wanafunzi STEMMUCO. Barua zitumwe kwenye anuani ya barua pepe ifuatayo superintendent.stemmuso@gmail.com Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 16, 2012. Upatapo tangazo hili umuarifu na mwenzako.

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais.
STEMMUCO.

Friday, September 7, 2012

ATTENTION TO ALL FIRST YEAR STUDENTS

Those who have been selected to join the various programmes in our University College and they would wish to have admission letters for permissions from their job stations and/or scholarship/sponsorship  purposes, you may send your inquiry to The Admissions Officer (Mr. Buteta) through the following numbers ; +255 (0) 655- 467-694, +255 (0) 767-467-694, +255 (0) 783 - 467-694 or by using the following e-mail addresses; buteta@yahoo.co.uk, buteta@stemmuco.ac.tz, admissions@stemmuco.ac.tz.

Karibu Sana!

SALLA, Donati P.
The STEMMUSO Vice President.

Re: THE OPENING DATES AT STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

This is to inform you Officially that, The following are the dates of opening the 2012/2013 Academic year in Our College:
1) All First year Students ( Certificates, Bachelor degrees, and Master  Students) they shall commence the 2012/2013 Academic year on Monday September 17, 2012.

2) The Continuing Students BASO2, & BASO3 Shall commence the 2012/2013 Academic year on Monday September 24, 2012.

3) The Continuing Students (BAED2, BAED3, BAPHILED2, BAPHILED3) Shall commence the 2012/2013 Academic year on Wednesday October 24, 2012.

SALLA, Donati P.
The STEMMUSO Vice President.