Wednesday, September 19, 2012

YAH: WANAFUNZI WALIOSHINDWA KUFANYA MITIHANI MAALUM NA YA KUJAZILIA (SPECIAL & SUPPLEMENTARY EXAMINATIONS)

Baada ya Kikao Cha Kamati ya taaluma ngazi ya Chuo kukaa na kuamua maamuzi yake Mnamo wiki iliyopita, kikao hicho kimeamua maamuzi yafuatayo kwamba, wale wote walioshindwa kufanya mitihani tajwa hapo juu kutokana na sababu mbalimbali watapewa nafasi ya kufanya mtihani husika mnamo mwezi septemba 2013 kwenye kipindi cha kufanya mitihani maalum na ya kujazilia. Pamoja na hayo wanafunzi wafuatao wawasiliane na Ndg. Clement Francis - Naibu Waziri wa Habari na Masuala ya Chuo ili waweze kupata barua zao zinazohusiana na tangazo hili. Unaweza kuwasiliana na Ndg. Clement Francis kwa namba zifuatazo 0717 521230.
Wanafunzi hao ni;-
1. MSANGI, Ridhwan E. BAED 15283.
2. NYARUBONA, Kassim BAED 15430
3. RUTEMBA, Issa H. BAED 15531
4. MWAKUBALI, Jophrey BAED 21666
5. MILANZI, David BAED 21589.
6. KAYEGEJI, Adam K. BAED 14929
7. JACKSON, Mussa BAED 14803.

ANGALIZO: Wahusika wa tangazo hili ni wale wenye tatizo tajwa kuanzia Mwaka wa Kwanza hadi Mwaka wa Tatu. Kwa Msaada zaidi wasiliana na Mwadili - Kitivo Cha Elimu kwa simu Namba 0715 86 43 79.

CLEMENT Francis 
NAIBU WAZIRI WA HABARI NA MASUALA YA CHUO.
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.

Saturday, September 8, 2012

YAH: KUTOLEWA KWA TAARIFA RASMI NA YA MWISHO KUHUSU MPANGILIO WA VITUO VYA KUFANYIA MAZOEZI YA UALIMU (TP ALLOCATIONS)


Hii ni kuwataarifu wanafunzi wote wa Mwaka wa Kwanza ambao wanatarajia kuingia Mwaka wa Pili, na wale wa Mwaka wa pili wanaotarajia kuingia Mwaka wa tatu katika Mwaka wa Masomo 2012/2013 katika  Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara kwamba, taarifa rasmi ya matokeo ya kupangwa kwenye vituo vya kufanyia mazoezi ya Ualimu (Teaching Practices) inapatikana katika wavuti ya Http://www.stemmuco.ac.tz hivyo basi unapaswa kufungua wavuti tajwa ili ufahamu ni wapi ulipopangwa kufanya Mazoezi ya Ualimu.
NB: (1)Hapatakuwepo na mabadiliko yoyote ya Kituo hivyo basi NENDA KWENYE KITUO ULICHOPANGIWA MOJA KWA MOJA. Pia hupaswi kuchelewa kwenye Kituo kwa sababu kama Mtathmini atapita katika kituo chako na akakukosa  utapaswa kurudia mwaka wa masomo kwani TP ni sehemu ya mtihani wa kitaaluma hapa Chuoni.
(2) Kwa tatizo lolote litakalo jitokeza wakati ukiwa kwenye mazoezi  unapaswa kuwasiliana na Mratibu wa eneo lako au kupiga namba za simu zifuatazo 0713 286 999, 0717 521230
, 0765 194 201. 
(3) Baada ya kumaliza Mazoezi unapaswa kuja Chuoni Moja kwa Moja kwa ajili ya Masomo kama ratiba inavyoelekeza. (Kwa Maelezo kuhusu tarehe za kufungua Chuo pekua katika Masjala ya wazi ya blogu hii).

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais.
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.

YAH: HOSTELI ZA CHUO.

Hii ni kuutaarifu Umma wa wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara kwamba Hosteli za Chuo katika mwaka wa masomo 2012/2013 ni kwa ajili ya Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza tuu na wale wanafunzi wenye Mahitaji maalumu. Hivyo basi wale walioshikilia vyumba kwa kuvifunga na kuondoka na funguo za vyumba husika wanapaswa kurudisha mara moja kwa Kiongozi Mwandamizi anayeshughulikia Masuala ya Udahili, Ukaribisho, na Makazi kwa namna yeyote ile na kwa haraka itakavyowezekana. Wale wanafunzi wenye mahitaji maalum watume barua za maombi ya kuishi hosteli kwenda kwa Mwadili wa Wanafunzi STEMMUCO. Barua zitumwe kwenye anuani ya barua pepe ifuatayo superintendent.stemmuso@gmail.com Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 16, 2012. Upatapo tangazo hili umuarifu na mwenzako.

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais.
STEMMUCO.

Friday, September 7, 2012

ATTENTION TO ALL FIRST YEAR STUDENTS

Those who have been selected to join the various programmes in our University College and they would wish to have admission letters for permissions from their job stations and/or scholarship/sponsorship  purposes, you may send your inquiry to The Admissions Officer (Mr. Buteta) through the following numbers ; +255 (0) 655- 467-694, +255 (0) 767-467-694, +255 (0) 783 - 467-694 or by using the following e-mail addresses; buteta@yahoo.co.uk, buteta@stemmuco.ac.tz, admissions@stemmuco.ac.tz.

Karibu Sana!

SALLA, Donati P.
The STEMMUSO Vice President.

Re: THE OPENING DATES AT STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

This is to inform you Officially that, The following are the dates of opening the 2012/2013 Academic year in Our College:
1) All First year Students ( Certificates, Bachelor degrees, and Master  Students) they shall commence the 2012/2013 Academic year on Monday September 17, 2012.

2) The Continuing Students BASO2, & BASO3 Shall commence the 2012/2013 Academic year on Monday September 24, 2012.

3) The Continuing Students (BAED2, BAED3, BAPHILED2, BAPHILED3) Shall commence the 2012/2013 Academic year on Wednesday October 24, 2012.

SALLA, Donati P.
The STEMMUSO Vice President.

Thursday, September 6, 2012

YAH: UTEUZI WA NDG. NG'HUMBUBANHU, Abel NA KUTUNUKIWA HATI YA UWAJIBIKAJI KATIKA SERIKALI KWA NDG: FRANCIS CLEMENT

Hii ni kuutaarifu Umma wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara kwamba, Mhe. Rais KAMILI, John C. wa Serikali ya Wanafunzi STEMMUSO amemteua Ndg. NG'HUMBUBANHU, Abel kuwa Kiongozi mwandamizi Ofisi ya Rais, kwa ajili ya kushughulikia Masuala ya udahili wa wanafunzi hapa Chuoni. Pia katika Shughuli zake za leo Mhe.Rais amemtunuku Ndg. Clement Francis hati ya Uwajibikaji katika Serikali, pamoja na kumteua rarsmi kama Msimamizi Mwandamizi wa Ustawi wa Wanafunzi na Chuo, katika Serikali ya Wanafunzi - STEMMUSO. Pamoja na hayo Mhe.Clement ataendelea kuwa Naibu Waziri wa Habari na Masuala ya Chuo huku akifanya kazi ya Usimamizi Mwandamizi katika ofisi ya Waziri Mkuu - STEMMUSO.
Mwisho Mhe.Rais amewapongeza viongozi hawa na kuwatakia kila kheri katika utekelezaji wa majukumu yao.

"Aluta Continua" Tuongeze jitihada katika kulijenga jiji la Mungu!

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.




YAH: MALIPO YA POSHO YA UTAFITI KWA WANAFUNZI WALIOMALIZA MWAKA WA TATU KATIKA MWAKA WA MASOMO 2011/2012

Hii ni kuwataarifu wanafunzi wote waliomaliza mwaka wa tatu Chuoni STEMMUCO katika mwaka wa masomo 2011/2012 kwamba, malipo ya posho ya kufanya utafiti ni shilingi 100,000/= TZS (Laki moja tu ya Kitanzania). Pia kwa mujibu wa kanuni za utoaji wa fedha za Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, ni kwamba haturuhusiwi kufanya malipo yoyote kwa Mwanafunzi ambaye hajasaini taarifa za uthibitisho wa kupokea malipo hayo. Hivyo basi wale wanachuo walimaliza masomo yao katika mwaka tajwa hapo juu, kama wapo jirani na Chuo wanashauriwa kufika hapa chuoni na kwenda moja kwa moja kwenye ofisi ya Mwadili wa wanafunzi kwa ajili ya kusaini malipo yao. Wale wanachuo ambao wapo mbali mnashauriwa kuwa watulivu hadi siku ya mahafali (ambapo ni mwezi Desemba) hivyo basi utakapokuja Chuoni kwa ajili ya Mahafali ndipo hapo utakaposaini na kulipwa malipo yako. Kama unaona kwamba unaweza kuja hapa chuoni na kusaini malipo yako basi hakuna kizuizi chochote kwani unaweza kuja ukasaini, kisha ukapewa malipo yako.

Ofisi ya Mwadili wa Wanafunzi pamoja Ofisi ya Waziri wa Mikopo - STEMMUSO, Kwa pamoja tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais
CHUO KIKUU CHA STELLA MARIS MTWARA.

Wednesday, September 5, 2012

HABARI MPASUKO (Breaking News)

Hii ni kuwataarifu Wanafunzi wote wa Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara ambao wanatarajia kuingia Mwaka wa pili na wa tatu katika mwaka wa masomo 2012/2013 na pia ni wafaidika wa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu - Tanzania  kwamba, leo Jumatano tarehe 05 Septemba 2012, fedha za posho kwa ajili ya Mafunzo kwa vitendo zimekwisha wekwa katika akaunti zenu. wale wenye matatizo mbalimbali yanahusu mikopo wanaweza kutuma taarifa za matatizo yao kupitia mikopo.stemmuso@gmail.com ili matatizo yao yaweze kutatuliwa. Kwa wanafunzi wa mwaka wa tatu wanaombwa kuwa na uvumilivu kidogo wakati Afisa Mikopo wa Chuo akiendelea kuandaa taratibu za kisheria kwa ajili ya Malipo yao.

Nawatakieni siku njema.

SALLA, Donati P.
Makamu wa Rais
STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

YAH: TANZIA YA KIFO CHA DEZDER DENICE

Uongozi wa Serikali ya Wanafunzi STEMMUSO unasikitika kuwataarifu juu ya kifo cha mwanafunzi mwenzetu aliyekuwa mwaka wa pili na kutaraji kuingia mwaka wa tatu 2012/2013 ambaye Jina lake ni DEZDER, Denice au kwa jina maarufu "Kaboy" kwamba amefariki usiku wa kuamkia Jumatatu tarehe 03 September 2012. Marehemu amezikwa kijijini kwao Rubya, Mkoani Kagera katika siku ya Jumanne tarehe 04 September 2012. Kwa upande wa Chuo, Chuo Kiliwakilishwa na Padre kutoka SAUT Main Campus na kwa upande wa serikali ya Wanafunzi, Tuliongozwa na Mhe: Deusdedith Mathius - Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi STEMMUSO. Chuo kilitoa rambirambi ya fedha taslimu kwenye familia ya marehemu na pia  baadhi ya wanafunzi wenzetu wa STEMMUCO waishio mkoani Kagera walihudhuria maziko hayo.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa! Jina la Bwana libarikiwe na Mungu ailaze roho ya marehemu pahala pema peponi Amen.

SALLA, Donati P.
Makamu wa  Rais
STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE.

Monday, September 3, 2012

RE:PHILOSOPHY OF EDUCATION (EF:112)

This is to inform all students who expect to seat for the Philosophy of Education (EF:112) as their Special/Supplementary Examination that, the aforesaid examination (EF:112) shall be done by tommorow Tuesday 04th September 2012 at MTR 7 From 16:00 Hrs to 19:00 Hrs. If you have got this information please may you inform your colleague.

SALLA, Donati P.
The STEMMUSO Vice President.

Sunday, September 2, 2012

YAH: MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STEMMUCO

Hii ni kuutaarifu Umma wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba, Majina ya watu waliochaguliwa kujinga na Chuo Kikuu Cha Stella Maris Mtwara katika programu mbalimbali yametangazwa jana rasmi na Afisa Udahili wa Chuo kupitia wavuti yetu ya www.stemmuco.ac.tz. Pia fomu za kujiunga na Chuo (Joining Instructions) zinapatikana katika wavuti hiyo ya www.stemmuco.ac.tz ikiwa ni pamoja na mchanganuo wa malipo ya ada. Kama wewe ni mmoja kati ya waliochaguliwa kujiunga na STEMMUCO, unapaswa kupakua (download) fomu inayokuhusu na kuijaza kwa umakini kisha kuja nayo hapa chuoni. Majina ya Wanafunzi waliochaguliwa katika Chuo Chetu ni wote kuanzia wale wa MBA (Master of Business Administration), Shahada ya Kwanza (Degree programmes), na Cheti katika fani mbalimbali.

SALLA, Donati P.
MAKAMU WA RAIS
STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE
 

RE: THE RELEASE OF 02ND SEMISTER RESULT OF THE YEAR 2011/2012 FOR THIRD YEAR STUDENTS.

The examination results of the second semester in 2011/2012 Academic Year have been released for third year students ONLY. These results include the results for students who are indebted by the college and those who have completed the payments of the tuition fees and all other required financial contributions. Recently the results are posted on the College noticeboard which is found in Dispensary area. You are advised to look for your relative and/or a friend who is present around the college, so that he/she may go and look for your results. Keep in mind that the supplementary and special examinations will be done starting from tomorrow Monday 03rd September 2012 up to Saturday 08th September 2012.

SALLA, Donati P.
The Vice President
Stella Maris Mtwara University College.